Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Sayyid Ali Sistani amejibu swali la kifiqhi kuhusu “kuficha kasoro ya bidhaa wakati wa kuiuza,” ambalo tunaliwasilisha kwa wasomaji na wenye shauku ya kufahamu hukumu hii.
Kuficha kasoro ya bidhaa wakati wa kuuza
Swali:
Je, muuzaji anapaswa kumweleza mnunuzi kuhusu kasoro iliyopo katika bidhaa? Ikiwa hatamweleza, hukumu ya kitendo chake na ya muamala huo itakuwaje?
Jawabu:
Ingawa kuficha kasoro si jambo linaloruhusiwa, lakini si lazima kuitaja kasoro hiyo. Hata hivyo, ikiwa hakuitaja kasoro hiyo na baadaye mnunuzi akaigundua, basi mnunuzi ana haki ya kuvunja muamala huo.
Maoni yako